H@ki Ngowi H@ki Ngowi
 Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa akimkabidhi Mfanyabiashara maarufu nchini, Mustafa Sabodo vibali vya ujenzi wa jengo hilo, kushoto ni  Mwenyekiti wa Madhehebu  ya Khoja Shia Shiraz Walji
--
MFANYABIASHARA maarufu nchini, Mustafa Sabodo ametoa zaidi ya sh.bilioni 5 kwa madhehebu ya Khoja Shia Ithnaashri Jamat kwa ajili ya kujenga jengo la maegesho ya magari.
 
Akizungumza katika hafla ya kupokea vibali vya ujenzi wa jengo hilo Dar es Salaam leo kutoka kwa Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa alisema jengo hilo litasimamiwa na madhehebu hayo.
 
Alisema jengo hilo lililopo katika mitaa ya India na Morogoro la ghorofa 14 litakuwa na uwezo wa kuhifadhi magari 180 kwa wakati mmoja.
 
Silaa alisema fedha zitakazopatikana kwa malipo ya maegesho ya magari katika kipindi cha miaka 10 zitafanya kazi ya kuchimba visima katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu.Meya alisema kwa muda mrefu Jiji la Dar es Salaam limekuwa likikabiliwa na maeneo ya kuegesha magari na kuwa jengo hilo la kwanza kubwa litakuwa ni mkombozi mkubwa.
 
"Kwa muda mrefu tumekuwa na matatizo ya kuegesha magari katika jiji letu hivyo msaada aliotoa ndugu yetu Sabodo kwa madhehebu hayo ya ujenzi wa maegesho hayo itasaidia sana kupunguza tatizo hilo," alisema Silaa.
 
Alisema Manispaa imepokea jambo hilo kwa mikono miwili na ndio maana imekamilisha vibali ili ujenzi huo uende pasipo kikwazo chochote.
 
Alisema jengo hilo litaitwa Sabodo Car Park jambo litakalo weka kumbukumbu ya mchango wake katika kufanikisha shughuliza za maendeleo.
 
Mwenyekiti wa Madhehebu hayo Shiraz Walji, alimshukuru Sabodo kwa msaada wake huo na kuahidi kusimamia vizuri mradi huo ambao utakuwa wa manufaa kwa Watanzania wote.
 Mhe. Peter Msigwa akiandika masuali yaliokuwa yakiulizwa na baadhi ya wakireketwa
 Mhe. Nassari Joshua (Dogo Janja) Akishanga mamia ya wana DMV waliofurika katika uzinduzi rasmi watawi la Chadema Washington Dc
 Mhe. Leticia Nyerere (Picha ya kwanza kushoto)akiwa kwenye uzinduzi wa watawi la Chadema Washington Dc
 Mhe. Maryam Msabaha akiwa kwenye uzinduzi wa watawi la Chadema Washington Dc
 Mwanachama wa chadema kutoka Boston Ma akiuliza masuali tafauti  katika mpango mzima wa uzinduzi rasmi watawi la Chadema Washington Dc uliofanyika jana Mei 27, kwenye ukumbi wa Mirage Hall uliopo University  Bld, Hysattsville, Maryland Nchini Marekani.
 Kamanda Doto akiuliza masuali tafauti  katika mpango mzima wa uzinduzi rasmi watawi la Chadema Washington Dc uliofanyika jana Mei 27, kwenye ukumbi wa Mirage Hall uliopo University  Bld, Hysattsville, Maryland Nchini Marekani.
 Mhe. Zitto Kabwe akitoa hutba kuelezea mpango mzima wa mambo yanavyoendelea nchini Tanzania
 Uongozi wa juu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  katika uzinduzi rasmi watawi la Chadema Washington Dc  kwenye meza ya juu wa kwanza kushoto Libe Mwangombe, akifatiwa na Mhe. Peter Msigwa,  Mwenyekiti wa tawi Mhe. Kalley Pandukizi,  Mhe. Zitto Kabwe, na Mhe. Nassari Joshua, Dogo Janja, mkutano huo ulifanyika kwenye ukumbi wa Mirage Hall uliopo University Of Bld, Hysattsville, Maryland Nchini Marekani.
 Wana DMV wakisikiliza hutuba ya Mhe. Zitto Kabwe.
Baadhi ya wakereketwa wachukua kadi baada ya uzinduzi wa tawi la chadema Washington.


 Bondia Iddy Mnyeke kushoto akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na Vitor Njait wakati wa mazoezi yanayoendelea katika kambi ya ngumi ya Ilala Mnyeke  anajitahalisha na mpambano wake dhidi ya Fadhiri Awadhi utakaofanyika June 9 katika ukumbi wa Frensi kona Manzese Dar es salaam .
  Bondia Iddy Mnyeke kushoto akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na Vitor Njait wakati wa mazoezi yanayoendelea katika kambi ya ngumi ya Ilala Mnyeke  anajitahalisha na mpambano wake dhidi ya Fadhiri Awadhi utakaofanyika June 9 katika ukumbi wa Frensi kona Manzese Dar es salaam .
  Mmiliki na Mwendeshaji wa Mtandao wa Lukaza Blog Mh Josephat Lukaza alipokua akitoa maelekezo jinsi ya Lukaza Blog inavyofanya kazi na vilevile Mtandao wa Lukaza Blog unavyopatikana na ulivyoweza kupokelewa Vizuri ndani ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) na vyuo vikuu tanzania wakati wa Maonyesho yaliyofanyika Chuoni hapo jana
  Mwanafunzi wa Mwaka wa 3 kutoka kitivo cha mawasiliano na kompyuta Mwinula Peter Kingamkono alipokua akionyesha na kutoa maelezo juu ya Mtandao wa Kijamii Wa Michezo ya Mtandaoni(Game Social Network) unavyofanya kazi katika maonyesho yaliyofanyika katika Ukumbi wa Chimwaga uliopo Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) jana
 Mmiliki wa Mtandao wa Lukaza Blog Mh Josephat Lukaza (Wa kwanza Kulia) akiwa katika Picha ya Pamoja na Wadau wa Lukaza Blog mara baada ya Kumalizika kwa Maonyesho hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Chimwaga uliopo Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) katikati ni Mh Mzagamba Thobias Kutoka Uswis na Wa Kwanza Kulia ni Atu Mwanafunzi wa Mwaka wa 3 UDOM.
  Mmoja wa wanakamati wa maandilizi ya maonyesho haya ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa 3 Bi Atu anayesoma shahada ya kwanza ya Mazingira ya Chuo Kikuu Cha Dodoma alipokua akitoa neno wakati wa maonyesho hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Chimwaga uliopo katika Chuo Kikuu cha Dodoma(UDOM) jana
 Wanafunzi wa UDOM wanaosoma shahada ya kwanza ya Filamu na Sanaa, Kiswahili wakionyesha uwezo wao wa kucheza boringo katika maonyesho yaliyofanyika jana Katika Ukumbi wa Chimwaga uliopo Chuo Kikuu Cah Dodoma (UDOM)
 Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Ambaye pia ni Mwanafunzi wa Shahaada ya kwanza ya Utalii ya Chuo Kikuu Cha Dodoma alipokua akitoa Burudani wakati wa maonyesho ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dodoma yaliyofanyika jana katika ukumbi wa Chimwaga uliopo Chuoni hapa
 Mmoja wa Wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sanaa na Filamu Babra Kalugira akiwa kwenye Kirekodi Video (VIDEO CAMERA) akichukua video ya matukio yaliyokuwa yakiendelea katika Maonyesho hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Chimwaga uliopo Chuoni Hapo
 Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dodoma waliohudhuria maonyesho hayo leo yaliyofanyika katika ukumbi wa Chimwaga uliopo Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM)
   Mwanafunzi wa Mwaka wa 3 anayesoma shahada ya kwanza ya filamu na sanaa anayejulikana kwa jina la wacko jacko akiwa amesimama pembeni mwa moja ya michoro aliyochora kwa Mikono yake na hapo alikua katika maonyesho yaliyofanyika chuo kikuu cha Dodoma jana
 Muandaaji wa Maonyesho haya Ester Zangi ambaye pia ni Mwanafunzi wa Mwaka wa 3 anayesomea shahada ya kwanza ya sayansi ya siasa na utawala wa umma(Wa Kwanza Kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dodoma ambao Wameonyesha vipaji vyao Vya Kuchora Michoro inayoonekana hapo katika maonyesho yaliyofanyika jana Chuo Kikuu Cha Dodoma katika Ukumbi wa Chimwaga
Ndugu zangu,

MFALME Suleiman aliambiwa ndotoni  aombe kitu chochote kwa Mola wake,  naye akajibu; “ Ewe Mola wangu, nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili ili niwahukumu watu wako, na kupambanua mema na mabaya, maana ni nani awezaye kuwahukumu hawa watu wako walio wengi?” Hivyo basi, Mfalme Suleiman aliichagua hekima. Maana, ni Mfalme Suleiman huyo anayekaririwa na vitabu vya dini akitamka, kuwa; “ Watu wangu wanaangamia kwa kukosa hekima”.

Naam, hekima ndilo jambo lililo bora kabisa kwa mwanadamu kuwa nalo. Mwanadamu aliyepunguwa hekima ana hasara kubwa maishani. Hekima ni  tunu na kipaji ambacho Mwenyezi Mungu amewajalia waja wake, ili nao waweze  kupambanua na kuamua kati ya yalo mema na maovu. Duniani hakuna shule ya hekima.

Zimetufika habari; Zanzibar kuna moto unawaka. Si moto wa kuupuza.  Hekima inatuongoza katika kutambua, kuwa ukiupuuzia moto unaowaka kwenye nyumba ya jirani yako, basi, nyumba yako pia imo hatarini kuungua . Naam, ndio sababu ya kusema; Jambo la Zanzibar ni letu.

Ndio, ni letu hata sie tulio bara.  msiba wa Unguja ni msiba wetu. Hivyo, kadhia hii ya Zanzibar ni kadhia yetu. Ni wakati  sasa wa kutanguliza busara na hekima katika kutanzua kadhia hii.  Hoja ya msingi inasemwa kuwa ni suala la Muungano. Mengine ni makandokando yanayotokana na hoja ya msingi. Basi, tuujadili Muungano, kisha tuone kama kuna lingine. Maana, hata bila Muungano wa Serikali moja, sisi bado ni ndugu na majirani wa daima na milele. Tujadili basi aina iliyo bora ya Muungano ili tuendelee kushirikiana kama ndugu.

Binafsi nilifika Zanzibar kwa mara ya kwanza mwaka 1988 ( pichani). Nilikuwa kijana mdogo sana. Zanzibar ndio kisiwa cha kwanza kupata kukitembelea. Tangu hapo niliipenda Zanzibar, nimefika Zanzibar mara kadhaa. Wenyeji ni wakarimu sana. Lakini, ukweli ni huu, tangu safari yangu ya kwanza Unguja miaka hiyo, wenyeji walinikumbusha, tena kwa kutamka kwa vinywa, kuwa mimi ni ' Mtanganyika'- mtu wa mlima. Hivyo, kwangu mimi, hoja ya Muungano nimeionja kwa karibu tangu mwaka 1988 nikiwa Zanzibar. 

Si jambo jema wala la kistaarabu kwa watu wachache kule Zanzibar kuchoma moto makanisa, baa na biashara za watu wa kutoka upande wa pili wa Muungano, lakini, vitendo hivi viovu vinavyopaswa kukemewa kwa nguvu zote haviwezi kumalizwa kwa nguvu za kipolisi au kijeshi, bali kwa kuzikutanisha pande zinazotofautiana kwenye meza ya mazungumzo.

Kwa hatua iliyopo sasa, bado Wazanzibari wenyewe wanaweza kukaa chini na kujadiliana kwa uwazi namna ya kwenda mbele. Lililo muhimu ni kuhifadhi amani na utulivu uliokuwepo.

Tayari kinachotokea Zanzibar kimeshakuwa na athari mbaya kiuchumi na kijamii. Kijamii, kuna mbegu za chuki zinapandwa. Ni jambo la hatari. Siku zote , chuki huzaa chuki, silaha huzaa silaha na hatimaye kupelekea uvunjivu wa amani wa muda mrefu. 

Katika dunia ya sasa ya teknolojia ya upashanaji habari, habari za uvunjivu wa amani Zanzibar zimeshasambaa duniani kote kama moshi wa kifuu. Watalii wa dunia wanataadharishwa sasa kutokwenda Zanzibar. Tunajua , baada ya kushuka kwa soko la karafuu, asilimia kubwa ya uchumi wa Zanzibar inatokana na mapato kwenye sekta ya utalii. Kadhia hii itapelekea kushuka kwa biashara ya utalii Zanzibar na hivyo kushuka kwa mapato.

Na mfano rahisi wa jinsi Mzanzibar wa kawaida atakavyoathirika, ni pale atakapoambiwa na wenye mahoteli asisitishe kupeleka samaki wake kwa vile wageni watalii wamehadimika. Na kuna vijana wengi wa Zanzibar ambao kipato chao kinategemea  sana shughuli za utalii. Nao watakosa cha kufanya, na mapato pia. Mazingira hayo huchangia kuongezeka kwa vitendo vya uhalifu. Na hasira pia ya wananchi, naam, midomo yenye njaa ni midomo yenye hasira. 

Kadhia ya Zanzibar inaweza pia kuathiri uchumi wa Bara hasa kwenye eneo hilo la utalii ukiachilia maeneo mengine. Mfano, kuna watalii wanaokuja Bara wakiwa na mipango ya kuunganisha safari zao hadi  Zanzibar. Kama Zanzibar hakuendeki na bara hakutaendeka pia. Hivyo, hata mapato ya bara yanayotokana na biashara ya utalii yatapungua.

Naam, huu si wakati tena wa kutanguliza propapanda. Ndio, propaganda iwekwe kando na diplomasia ichukue nafasi yake; mazungumzo, mazungumzo, mazungumzo.  Ndicho kinachohitajika sasa. Pande mbili zinazokinzana ziwe kwenye mazungumzo hadi zifikie muafaka ulio na maslahi kwa jamii pana.

Huu si wakati wa kutafuta mshindi, maana, hata tulipofikia sote tumeshashindwa. Ni wakati wa kutanguliza busara na hekima. Na maamuzi mengine tunayotakiwa kuyafanya sasa yasitokane na mazoea ya siku nyuma bali uzoefu mpya tunaoupata sasa.

Na hilo ni Neno La Leo.

Maggid Mjengwa,
Iringa.

0788 111 765
 Meneja Mahusiano na Mawasiliano ya Jamii wa TBL,Edith Mushi afafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi rasmi wa Bia ya Kopo ya Castle Lite jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Meneja wa Bia ya Castle Lite,Pameka Kikuli.
 Meneja wa Bia ya Castle Lite,Pameka Kikuli akionyesha kopo mpya zilizojazwa Bia hiyo ikiwa ni muendelezo wa kuwarahisishia wanywaji wake kuondoka nayo,wakati wa uzinduzi rasmi uliofanyika leo kwenye kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),Ilala Mchikichini jijini Dar es Salaam.Kulia ni Meneja Mahusiano na Mawasiliano ya Jamii wa TBL,Edith Mushi.
--
 
Bia maarufu ya Castle Lite, inayozalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) leo imezindua rasmi muonekano wa kopo lililojazwa kinywaji hicho ikiwa ni muendelezo wa kuwarahisishia walaji upatikanaji wa Bia hiyo iliyotokea kupendwa na watumiaji wa vileo na kuifanya iwe bia inayokua kwa kasi hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi huo, Meneja wa Bia ya Castle Lite Bi. Pamela Kikuli alisema; Leo tunazindua ujazo mpya wa bia ya Castle lite, bia yenu muipendayo kwa sasa inapatikana katika kopo lenye ujazo wa mililita 330. Uamuzi huu unatokana na mahitaji makubwa toka kwa watumiaji na wapenzi wa bia hii ambayo imekuwa ikipatikana katika chupa yenye ujazo wa mililita 375.

 Wateja wetu walihitaji kuipata bia yao popote pale walipo au kuwa nayo popote waendapo, hivyo kupatikana kwa bia hii katika chupa peke yake kulipunguza uhuru wa kuwa na bia yao popote waendapo kwani walihitaji kurudisha chupa kila waitumiapo.

Uzinduzi wa Castle lite ya kopo utasaidia zaidi kuongeza upatikanaji wa kinywaji hiki katika maduka ya reja reja (super markets) n.k kote nchini na kuwapa nafasi wapenzi wa castle lite kununua bia yao waipendayo na kwenda nayo nyumbani. Bei ya reja reja kwa kopo ni shilingi 1700/- na bei ya reja reja kwa chupa itaendelea kubaki ile ile 1700/-.

Kwa upande wake Meneja mawasiliano na mahusiano ya jamii wa Tbl Edith Mushi aliwashukuru wapenzi na watumiaji wa bia ya Castle Lite kwa kuweza kuipa mafanikio makubwa katika soko la bia hapa nchini, “ninawahakikishia kuwa mnafanya uamuzi ulio sahihi kwa kuchagua kutumia Castle Lite” nasi tutaendelea kuwapatia bia iliyo bora siku zote. Alisema Edith.
 Mohammed Aboud Mohammed,  Waziri wa Nchi,  Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Zanzibar.
---
Itakumbukwa kwamba tarehe 25 Aprili, 2012 Kamati Maalumu ya Mawaziri ilikutana na viongozi wa jumuiya ya Uamsho, Maimamu na Masheikh kuzungumzia hali iliyojitokeza nchini katika kufanya mihadhara ambayo ilikuwa inaashiria uvunjifu wa amani.

Katika kikao hicho Serikali iliwataka Viongozi hao wanapofanya mihadhara na mikutano inayohusu masuala ya maoni ya katiba wafuate taratibu zilizowekwa kisheria.

Aidha, Serikali iliwasihi viongozi hao kuepuka matumizi ya lugha na vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani katika nchi yetu na iliwataka pale ambapo wana maoni yoyote kuhusu Serikali wafuate taratibu zilizowekwa na Serikali itakuwa tayari kuzungumza nao ili kuwa na mustakabali mwema katika nchi yetu.

Vile vile, kupitia taarifa maalumu ya Serikali iliyotolewa Aprili-Mei mwaka huu, Serikali ilieleza wazi kwamba tume ya marekebisho ya katiba imezinduliwa rasmi na kuwataka wananchi, taasisi na vikundi mbali mbali nchini vyenye nia ya kutaka kuelimisha umma kuhusu marekebisho ya katiba kufuata muongozo wa sheria namba 8 ya mwaka jana kama ilivyorekebishwa na sheria namba 2 ya mwaka huu 2012.

Kwenda kinyume na sheria hii ni kosa la jinai na hivyo iliwataka Wananchi wote kujiepusha na vitendo vyote vinavyokwenda kinyume na matakwa ya sheria.

Ndugu Wananchi, mbali na juhudi hizo za Serikali, bado wapo watu wachache wasioitakia mema nchi yetu na umoja uliopo wanaendeleza kwa makusudi vitendo vya kuvunja taratibu za sheria jambo ambalo limepelekea Jeshi la Polisi kuchukua hatua za kisheria.

Ndugu Wananchi, Serikali imesikitishwa na vitendo vilivyojitokeza vya vurugu na uvunjifu wa amani ambavyo vimeelezwa kwa kina na Jeshi la Polisi iliyotolewa mapema leo tarehe 25.05.2012 na Kamishna wa Polisi Zanzibar.

Kutokana na hali hiyo, Serikali inawahakikishia Wananchi wote kwamba itaendelea kudhibiti vitendo vyovyote vya uvunjifu wa sheria vinavyoashiria kuondolea nchi yetu amani na utulivu uliopo.

Ndugu Wananchi, Serikali inawahakikishia Wananchi kwamba Jeshi la Polisi litaendelea kuchukua hatua zifaazo ili kuwahakikishia usalama wa raia na mali zao unakuwepo na hali inaendelea kuwa shuwari, amani na utulivu.

Ndugu Wananchi, bado Serikali inasisitiza na kuwaomba wananchi wote waunge mkono juhudi za Serikali na kuacha kabisa kujiingiza katika vitendo ambavyo vinaashiria uvunjifu wa amani na utulivu katika nchi yetu.

Hivyo, tunawaomba Wananchi waendelee na shughuli zao kama kawaida na Serikali itaendelea kuwahakikishia usalama wao.

Aidha, Serikali inawaomba wazazi kuwadhibiti vijana wao wasijiingize katika vitendo viovu na vurugu kwani Jeshi la Polisi na Vikosi vyote vya Ulinzi na Usalama vitakuwa macho kupambana na vurugu hizo na vitendo vyote vya uvunjifu wa amani.

Kwa madhumuni ya kudhibiti amani na utulivu na usalama wa Wananchi wetu, Serikali katika kipindi hiki itachukua hatua zifuatazo:
  1. Inakataza mikusanyiko ya aina mbalimbali, maandamano, na mihadhara ya aina mbalimbali ambayo haijapata kibali cha Serikali.
  2. Serikali inaliagiza Jeshi la Polisi kuwatafuta na kuwafikisha katika vyombo vya sheria wale wote waliohusika na kufanya fujo zilizotokea katika maeneo mbali mbali ya Zanzibar
  3. Serikali inakemea vikali vitendo vyote vya hujuma na uharibifu wa amali zilizofanywa katika taasisi za umma, dini na mali za watu binafsi.
  4. Serikali inawapa pole Wananchi na Taasisi zilizoathirika na vurugu hizo na kuwahakikishia kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wale wote waliohusika katika kadhia hiyo.

Na mwisho, tunawaomba wananchi kushirikiana na Serikali kwa kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi pale ambapo itaonekana zipo dalili za uvunjifu wa amani katika maeneo yao.

Ahsanteni.

Nawashukuru kwa kunisikiliza.


Mohammed Aboud Mohammed, 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, 
Zanzibar.
 Naibu Mkurugenzi DPP-Stanslaus Boniface
---
MKURUGENZI Msaidizi wa ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini, Stanslaus Boniface Makulilo (44) ‘Jembe’ amefariki ghafla usiku wa kuamkia jana katika Hospitali ya Regency jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Mashitaka nchini(DPP), Dk.Eliezer Feleshi alilithibishia leo asubuhi kutokea kwa kifo hicho ambapo alisema bado ofisi yake na taifa limepata pigo kubwa lakuondokewa na gwiji hilo la uendeshaji wa mashitaka hususani ya jinai hapa nchini na kwamba mchango wake mzuri katika uendeshaji wa kesi hususani za jinai hautasaulika na utaenziwa.

 Dk.Feleshi alikuwa akizungumza kwa uzuni alisema Jumamosi jioni Boniface ambaye pia alikuwa Msimamizi wa Uendeshaji wa Kesi zenye maslahi kwa umma, aliingia Dar es Salaam, akitokea Moshi kwaajili ya kutoa mafunzo ya jinsi ya uendeshaji wa mashitaka kwa maofisa wa Idara ya Uhamiaji akiwa mwenye afya njema na alirejea nyumbani kwake Kinondoni lakini ilipofika usiku wa siku hiyo hali yake ilibadilika ghafla na kukimbizwa katika Hospitali ya Regency kwaajili ya matibabu.

 “Baada ya kufikishwa hospitalini hapo alifariki dunia ila mimi kama kiongozi wake wa kazi kwa sasa siwezi kusema chanzo cha kifo hicho hadi pale tutakapopata taarifa rasmi za madaktari na msiba upo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mtaa wa Sinza Load Kitalu Na.4 na hadi kufikia leo utaratibu shughuli za msiba zitakuwa zimefahamika na tutawajulisha”alisema Dk.Feleshi. Dk.Feleshi alimuelezea Boniface kuwa ni miongoni mwa mawakili wa serikali waliokuwa wakijitoa kwa moyo wao wote katika kuitumikia serikali yao katika uendeshaji wa kesi bila woga na katika kuthibitisha hilo ni katika kesi za mauji yaliyoibuika miaka ya nyumba mkoani Mbeya ambapo watu walikuwa wakiwachunya binadamu wenzao ngozi, kesi za wizi wa fedha za EPA, matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuongeza kuwa marehemu alikuwa akitumia taaluma yake kwa kuwapatia watu wengine waliokuwa wakiitaji.

 Miongoni mwa kesi kubwa ambazo mwandishi wa habari hizi amekuwa akimshuhudia akiziendesha kwa zaidi ya miaka mitano katika mahakama mbalimbali hapa nchini sasa ni kesi ya wizi wa shilingi bilioni 1.8 katika EPA, iliyokuwa ikimkabili Kada wa CCM, Rajabu Maranda na Farijala Hussein ambapo mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Mei 23 mwaka jana, iliwahukumu kwenda jela miaka mitano, kesi ya kula njama na kuomba rushwa ya shilingi milioni 10 iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la TBC, Jerry Murro na wenzake ambapo Murro alishinda kesi hiyo mwaka jana, kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na mfanyabishara Jayankumar Patel “Jeetu Patel’ na wenzake dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, DPP na Reginal Mengi iliyokuwa akitaka afutiwe kesi zake nne za EPA zilizopo katika mahakama ya Kisutu kwasababu Mengi alimuhukumu kabla ya hajahukumiwa na mahakama kwa sababu alimuita ni Fisadi Papa, ambapo Boniface alimwakilisha AG na DPP na aliibuka mshindi katika kesi hiyo.

 Kesi nyingine kubwa ambayo marehemu alikuwa akiziendesha ambazo bado hadi umauti unamkuta hazijatolewa hukumu ni ile ya mauji ya Ubungo Mataa ambayo inaendelewa kusikilizwa na Jaji Projestus Rugazia, rufaa ya kupinga hukumu ya mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliyomwona mfanyabiashara Naeem Gile ambayo inasikilizwa mbele ya Jaji Laurence Kaduri ambaye alikuwa akikabiliwa na makosa ya kutoa taarifa za uongo kuhusu kampuni ya kufua umeme ya Richmond LCC, kuwa hana kesi ya kujibu, rufaa ya kupinga hukumu ya mahakama ya Kisutu iliyomuona Jerry Murro hana hatia na kesi ya matumizi mabaya na kuisababishia serikali hasara ya shilingi bilioni 11.7 inayomkabili waliokuwa mawaziri wa Fedha na Nishati, Basil Mramba, Daniel Yona na Gray Mgonja. Boniface alizaliwa Februali 21 mwaka 1968 ameacha mke na watoto watatu, aliitimu shahaha ya kwanza ya Sheria mwaka 1995 na shahada ya pili ya sheria alimaliza mwaka 2008 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

 Julai Mosi mwaka 1995 aliajiriwa rasmi katika ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali kama Wakili wa Serikali, ilipofika Oktoba Mosi mwaka 2006 alipandishwa cheo na kuwa Wakili wa Serikali Mwandamizi.Oktoba Mosi mwaka 2007 alipandishwa cheo tena na kuwa Wakili Kiongozi wa Serikali. Nyadhifa ambazo Boniface aliwahi kuzishika enzi za uhai wake ni kati ya mwaka 2003-2007 alikuwa ni Wakili wa Serikali Mfawidhi Mkoa wa Mbeya

.Kati ya Mei 2007 na Oktoba 2010 alikuwa Wakili wa Serikali Mfawidhi Kanda ya Mwanza.Novemba 2009 hadi Novemba 2010 alikuwa Mwanasheria Mfawidhi wa Serikali mkoani Dar es Salaam. Kutokana na utendaji kazi wake mzuri ilipofika Desemba 2010 hadi mauti yanamkuta aliteuliwa kushika wadhifa wa Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha uendesha mashitaka na pia awaka Msimamizi wa uendeshaji kesi zenye maslahi kwa umma. Bwana alitoa na bwana ametwaa jina lake liimidiwe.

Mbunge wa kigamboni(CCM)Dr Faustine Ndugulile
--
Hivi karibuni nimekuwa nikipokea malalamiko mengi ya kukatika mara kwa mara kwa umeme katika maeneo ya Kigamboni na Mbagala.
Matatizo haya yanatokana na sababu kuu mbili: Moja, miundombinu ya umeme kuzidiwa na mahitaji na pili, uchakavu wa miundombinu.
Kwa hivi sasa, watumiaji wa umeme wa Kigamboni, Mbagala na Mkuranga wanapata mahitaji toka kwenye kituo kidogo kilichopo Ilala. Umeme unaotoka kwenye kituo hautoshelezi mahitaji ya maeneo yote yaliyotajwa hapo juu. Hali hii imepelekea baadhi ya maeneo kuwa na umeme ndogo na baadhi ya maeneo kukatika hususan nyakati za usiku.
HATUA ZINAZOCHUKULIWA KUTATUA TATIZO HILI
Hatua za muda mrefu:: Tanesco inatarajia kujenga Sub-station kubwa maeneo ya Mbagala ambayo itahudumua maeneo ya Kigamboni na Mbagala. Kazi hii inatarajia kuanza karibuni baada ya kukamilisha zoezi la fidia kwa wananchi waliobaki.
Hatua za muda mfupi: Tanesco inaendelea na ukarabati wa mfumo uliopo ili uweze kuihimili mahitaji ya sasa. Katika wiki hii, Tanesco ilikata umeme tarehe 22, 24 na leo 27 kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa kumi na mbili jioni ilikufanya kazi hii. Kwa mujibu wa Tanesco kazi hii inatarajia kukamilika wiki mbili zijazo.
Naomba tuvute subira wakati Tanesco wanalifanyia kazi tatizo la umeme kukatika mara kwa mara.
Ahsanteni.
Dkt.Faustine Ndugulile
Mbunge Kigamboni
Kiongozi wa Jumuiya ya kikundi cha uamsho, Sheikh Farid Hadi Ahmed
 Mmoja wa waandamani wa Kundi la Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam (JUMIKI) Kisiwani Unguja,Zanzibar akionyeshan kitambaa kilicho na Damu mapema leo Asubuhi wakati wakiendelea na maandamano yao ambayo yamesababisha vurugu kubwa kisiwani humo,iliyopelekea kuchomwa moto kwa moja ya makanisa pamoja baadhi ya magari yaliyokuwa yameengeshwa karibu na njia wapitazo.vurugu hizo zimeanza jana usiku baada ya kukamatwa kwa kiongozi wa Juimuiya hiyo
 Maelfu wa wazanzibari wakiongozwa na Taasisi za Kiislamu na Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) wakifanya matembezi ya amani katika barabara za Zanzibar na kupeleka ujumbe wao kwa viongozi wa serikali za Zanzibar na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Umoja wa Mataifa wakitaka Zanzibar huru ambapo baadhi ya watembeaji hao wakiongoza na Kiongozi wa Jumuiya hizo, Sheikh Farid Hadi Ahmed na viongozi wengine
 Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) liliopo mtaa wa Kariakoo mjini Unguja limechomwa moto jana usiku wa kuamkia leo na watu wasiojulikana
 Gari la Kiongozi wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Bishop Dickoson Maganga lililochomwa moto usiku wa jana katika eneo la Kariakoo nje ya kanisa hilo ambapo uharibifu wote unaelezwa kuwa umegharimu shilingi millioni 120.
 Gari la Kiongozi wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Bishop Dickoson Maganga
lililochomwa moto na watu wasiojulikana usiku wa leo katika eneo la Kariakoo nje ya kanisa hilo ambapo uharibifu wote unaelezwa kuwa umegharimu shilingi millioni 120.
 Kikosi cha Kuzuwia Fujo FFU kikizunguka kikiwa kimejihami katika maeneo ya Michenzani ambapo tayari jeshi la polisi limepiga marufuku mikusanyiko yoyote Mjini hapa
Katibu wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) Sheikh Abdallah Said Ali ambaye ni miongoni mwa wanaotafutwa na jeshi la polisi akizungumza na Radio DW asubuhi mapema kabla ya taarifa ya kutafutwa kwao kutolewa kwa vyombo vya habari
---
Maelfu ya wazanzibari leo wamefanya maandamano amani kuishindikiza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuitisha kura ya maoni juu ya Muungano na kupeleka ujumbe kwa Umoja wa Mataifa wa kutaka Zanzibar kujitenga kama ilivyofanya Sudan ya Kusini.

Wazanzibari hao wakiongozwa na Sheikh Farid Hadi Ahmed walitembea kutoka viwanja vya Lumumba na kupitia barabara ya Kinazini, Mpigaduri, Michenzani Maskani ya CCM Kisonge, kwa Biziredi na kurudi tena viwanja vya Lumumba.

Maandamano hayo walioyaita matembezi ya amani yalifanyika na kuhudhuriwa na maelfu ya wazanzibari ambapo awali kuliandaliwa kongamano kubwa lililoandaliwa na Taasisi za Kiislamu kwa kushirikiana na Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) kwa lengo la kuzungumzia mfumo wa elimu Zanzibar.

Akizungumza na maelfu ya wazanzibari kabla ya kuanza maandamano hayo yaliitwa ni matembezi ya amani, Sheikh Farid alisema wazanzibari wana haki kama walivyokuwa na haki wananchi wengine ulimwenguni kote kudai haki yao ndani ya nchi yao.

“Sisi wazanzibari kama wananchi wengine wowote duniani tuna haki ya kikatiba kudai nchi yetu kama walivyodai Sudan ya Kusini, mbona Sudan ya wameweza kujitenda na kupata nchi yao kwa nini sisi kama wazanzibari tusikubaliwe kudai nchi yetu sasa sisi tunampelekea salam katibu mkuu wa umoja wa mataifa kumwambia kuwa wazanzibari sasa wanataka nchi yao” alisisitiza Sheikh Farid huku akiungwa mkono kwa mamia hao kuinua mikono na kusema ndiooooo.

Awali Sheikh Farid alisema salamu hizo anataka zimfikie Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Kin moon ambaye kwamba wazanzibari wamechoshwa na kuwepo ndani ya Muungano ambao umedumu kwa miaka 48 lakini bado ukiwa na kero nyingi na malalamiko ambayo yanaonekana utatuzi wake ni mdogo na usiowezekana ambapo alisema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hauna manufaa yena na wazanzibari.

Katika kuonesha kwamba hawataki tume ya katiba ije kuchukua ya maoni ya katiba mpya Sheikh Farid alisema wanataka kwanza kuamuliwe suala la Muungano kabla ya jambo lolote na kuahidi kwamba wataendelea kufanya makongamano, mihadhara na maandamano kwa kadiri wawezavyo hadi hapo serikali itakaposikia kilio hicho.

“Ujumbe huu tunautoa kwa Ban Kin moon, na kwa ulimwengu mzima lakini pia tunataka rais wetu Dk Shein asikie kilio hiki na Rais Kikwete ambaye yeye ni mtetezi wa haki za binaadamu na pia ni mfuatiliaji wa nchi zinazovunja haki za binaadamu tunataka asikie kilio cha wazanzibari kuwa wanataka nchi yao” alisema. 

Alisema juzi wamefanya maombi maalumu ya kumuombea Rais wa Zanzibar lengo likiwa ni kumjaaliwa kheri na awe na maamuzi sahihi juu ya wananchi wa Zanzibar sambamba na kuwaomba Makamu wa Kwanza na makamu wa Pili wa Zanzibar kusikia kilio cha wazanzibari wasiotaka Muungano.

“Tunamuomba Rais wetu Dk Shein, Makamu wa Kwanza Maalim Seif na Makamu wa Pili Balozi Seif kwamba sisi wazanzibari tunahitaji Zanzibar huru, tunahitaji heshima ya nchi yetu na tupo tayari kwa lolote kwa hivyo tunataka salamu hizi na ujumbe huu ukufikieni” alisema Sheikh Farid huku akiungwa mkono na maelfu waliohudhuria katika kongamano hilo ambalo awali liliandaliwa kwa lengo la kuzungumzia masuala la elimu na mfumo wake.

Akiendelea kutoa salamu hizo mara Sheikh Farid alisoma kifungu cha 16 cha katiba na kuwaleza wananchi kwamba haki ya kutembea ni haki ya kila mwananchi ambayo imeainishwa katika katiba na sheria za haki za binaadamu hivyo aliwageukiwa na kuwataka wasimame na kisha kumfuata yeye.

“Haki ya kutembea ni haki ya msingi kwa mujibu wa sheria na kifungu cha 16 kinatupa haki ya kutembea sasa mimi nataka kutembea jeee mpo tayari kutembea na mimi? Alihoji Sheikh huyo huku akijibiwa na umma mkubwa kwamba ndioooo”

Aliongeza kwamba “Tunaanza kutembea na tuone mtu atukamate tunakwenda njia ya kinazini, tunapita michenzani, tunapita barabara ya kwa biziredi na kisha tunarejea hapa hapa kuendelea na kongamano letu kwa amani kabisa mmesikia….akajibiwa ndiooooo”
baada ya kusema hivyo Sheikh Farid alitoa takbir na kuanza kukamatana mikono na viongozi wenzake na huku ummati mkubwa ukiwa umekamatana mikono nyuma na kuanza safari kwa pamoja na kutembea katika barabara ambazo walizitaja awali.

Waandamani hao walikamata mabango yenye maandishi mbali mbali ikiwemo hatutaki muungano, tunataka nchi yetu, zanzibar bila ya muungano inawezekana na wengine kadhalika huku wakitembea njiani na kupiga takbir ambapo walikuwa wakisema Mwenyeenzi Mungu Mkubwa, Mwenyeenzi Mungu Mkubwa sisi hatuna uwezo isipokuwa tunakutegemea wewe Mwenyeenzi Mungu.

Waandamanaji hao walianza kutembea kwa utaratibu maalumu huku magari yakisimama na kuwapisha bila ya kuwepo jeshi la polisi ambapo viongozi wa jumuiya hiyo na wananchi wengine waliongoza utaratibu huo na kutembea katika barabara kwa utaratibu mzuri hadi kumaliza maandamano yao waliyoyaita matembezi ya amani. 

Baadae jeshi la polisi lilifika katika eneo ambalo kumefanyika maandamano hayo na kufungua mabango yao ya kuwataka watu kuondoka lakini wakati magari hayo ya polisi matatu yanafika eneo hilo la Kariakoo tayari ummati mkubwa ulikuwa umeshapita katika eneo hilo na hivyo kuingia ndani ya magari yao na kuondoka kwa salama.

Awali akitoa mada katika kongamano hilo, Maalim Abdulhafidh Malelemba alisema sekta ya elimu imekuw aikidorora Zanzibar kutokana na kukandamizwa na mambo ya Muungano ambapo kila mwaka wanafunzi wanapofanya mitihani kufelishwa kwa makusudi huku idadi ya wanafunzi wanaokwenda katika vyuo vikuu wakiwa kidogo kutokana na kufelishwa katika mitihani ambapo husainiwa na baraza la mithani Tanzania (NECTA).

Wakizungumza katika nyakati tofauti katika kongamano hilo, baadhi ya walimu walisema kukosekana kwa baraza la mitihani Zanzibar kusimamia mitihani ya elimu ya juu ndio sababu ya wazanzibari kufelishwa kwa wingi na kushindwa kuingia katika vyuo vikuu kwa kuwa wanafunzi wengi wa Zanzibar hufelishwa.


Walimu hao walitoa ushahidi wa hivi karibuni wa kufelishwa wanafunzi wa kidatu cha nne ambapo walisema lile ni tukio la makusudia lililofanywa na baraza la mitihani ikiwa ni kuwadhoofishwa wanafunzi wa Zanzibar ili wasiendelee katika masomo kwa kuwafelisha.
----

JUMUIYA YA UAMSHO NA MIHADHARA YA KIISLAMU

(JUMIKI)

للجنة الدعوة الإسلامية

THE ASSOCIATION FOR ISLAMIC MOBILISATION AND PROPAGATION

P. O. BOX: 1266 -Tel:             +255-777-419473 begin_of_the_skype_highlighting            +255-777-419473      end_of_the_skype_highlighting       / 434145- FAX +255-024-2250022 E-Mail: jumiki@hotmail.com

MKUNAZINI ZANZIBAR


Tarehe 27MAY2012 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 

Kila sifa njema anastahiki ALLAH (S.W) na Rehma na Amani zimuendee Mtume Muhammad (S.A.W), ahli zake, Maswahaba zake na walio wema katika Uislamu.

Jumuia ya UAMSHO inatoa taarifa rasmi kwa umma wa Wazanzibari na Watanzania wote kwa ujumla kwamba haihusiki na vitendo vyote vya uvunjaji wa amani vilivyotokea usiku wa tarehe 26 Mei 2012. Kama alivyosema Mtume (S.A.W) katika Hijatul Wadaa, kwamba ni haramu kumwaga damu zenu, kuharibiana mali zenu, kuvunjiana heshma zenu ila kwa haki ya Uislamu (maana yake pale mtu anapofanya kosa na likathibitika atahukumiwa kwa hukmu ya Kiislamu). Vile vile Uislamu unaheshimu nyumba za ibada (Makanisa, Mahekalu na n.k) zisivunjwe wala zisiharibiwe.

Jumuia inatoa wito kwa Waislamu na Wazanzibari wote kuendelea kudumisha amani na utulivu wa nchi na kutoharibu mali za serikali, mali za wananchi, mali za taasisi za dini zenye imani tofauti, kwani kufanya hivyo ni kwenda kinyume na mafundisho ya dini ya Kiislamu. Jumuiya inayachukulia matukio yaliyotokea usiku wa jana, na yanayoendelea tangu alfajiri leo, kama ni njama za makusudi za wale wasioipendelea amani nchi hii, pamoja na kutaka kuipaka matope jumuiya na kutaka kuzuia lengo la Wazanzibari kudai nchi yao.

Tunatoa wito kwa Jeshi la Polisi na Vyombo vyote vya Dola wafanye kazi zao kama wanavyotakiwa kwa mujibu wa muongozo wa haki za binadamu kwa Polisi na vikosi vingine unaosema kwamba polisi na vyombo vingine vya dola wana jukumu la kutunza amani na utulivu na jukumu la kutoingilia haki za watu. Kila mtu anayo haki ya kuwekewa mazingira muafaka ya kitaifa na kimataifa yatakayomuwezesha kupata haki zake za binadamu.

Polisi na vyombo vingine vya dola wana jukumu la kutunza amani na utulivu na jukumu la kutoingilia haki za watu isipokuwa tu kwa minajil ya kulinda haki za wengine.

Polisi na vyombo vingine vya dola wana jukumu la kuheshimu, kulinda na kutetea haki za binadamu kwa watu wote.

WABILLLAH TAWFIQ .
 Mheshimiwa Balozi wa Botswana, Bwana Roy Blackbeard, akihutubia katika sherehe za kuadhimisha siku ya Afrika.
Mheshimiwa Balozi wa Uganda, Mama Joan Rwabyomere, akifungua Maadhimisho ya siku ya Afrika hapa nchini Uingereza, katika sherehe ambazozilifanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Lagham Palace, London.
 Dada Jestina George na dada Rahma Lupatu, wakijivunia Utanzania wao katika sherehe hizo za siku ya Afrika
Kutoka kulia, Dada Rahma Lupatu, Caroline Chipeta, Bwana David Nginila, Bwana Kiondo (maafisa wa Ubalozi wa Tanzania, London) na Dada Jestina George, maarufu kama Queen wa Blog hapa Uingereza.
 Kikundi cha ngoma kutoka Ghana, wakitoa burudani katika sherehe za kuadhimisha siku ya Afrika hapa London
 Mabalozi ,Maafisa wa Ubalozi na wawakilishi kutoka nchi mbalimbali za Afrika na wageni waalikwa katika sherehe hizo.
--
Siku ya Afrika iliadhimisha rasmi jana hapa nchini Uingereza kwa kujuisha nchi zote za Afrika zenye Balozi au Wawakilishi wao hapa nchini Uingereza. Katika sherehe hiyo rasmi ya kuadhimishwa kwa Siku ya Afrika, kulitolewa hotuba na Balozi wa Botswana na mbaye ni Mkuu wa Mabalozi wa nchi za Afrika hapa Uingereza, Mheshimiwa Roy Warren Blackbeard.

Aidha Mheshimiwa Balozi Roy Blackbeard, alitoa salamu maalum kutoka kwa mwenyekiti wa sasa wa Umoja wa nchi za Afrika, Mheshimiwa Yayi Boni, ambaye pia ni Raisi wa Benin.

Balozi Roy, alielezea changamoto nyingi zinazo tokea Barani Afrika na kwingineko na juhudi maalum zinazofanywa na Jumuiya ya Umoja wa nchi za Afrika kutatua migogoro na matatizo ya mara kwa mara yanayolikumba Bara letu la Afrika.

kabla ya kutolewa hotuba hiyo, Balozi wa Uganda Mheshimiwa Mama Joan Rwabyomere, alifungua kwa kuwakaribisha Mabalozi, Wawakilishi, Marafiki wa Afrika na Wageni mbalimbali waalikwa na kuwashukuru kwa kufika kwao na kujumuika pamoja na waafrika wote duniani kuadhimisha siku hiyo hapa nchini Uingereza. Amani, Upendo, Ushirikiano na Mshikamano miongoni mwa nchi za Afrika vilihimizwa katika maadhimisho hayo.
  Makamu wa Rais wa Jahmuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwahutubia wageni waalikwa na wanachama wa CCM, waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa vitabu viwili vya Binadamu na Kazi na Ukweli kwa mujibu wa Biblia, na Kurani Tukufu, Suna za Mtume  na Sheria za nchi, vilivyotungwa na Katibu Mkuu Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Yusuph Makamba. Hafla hiyo iliyofanyika leo Mei 27, 2012 katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, imefanyika sambamba na hafla ya kumpongeza kwa kuitumikia nafasi yake ya Katibu Mkuu wa CCM hadi anastaafu
 Makamu wa Rais wa Jahmuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,akikata utepe kuzindua kitabu cha Ukweli kwa Mujibu wa Biblia, Kuran Tukufu, Suna za Mtume na Sheria za Nchi, kilichotungwa na Katibu Mkuu Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Yusuph Makamba (kulia) wakati ya uzinduzi huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo Mei 27, 2012, sambamba na hafla ya kumpongeza kwa kuitumikia nafasi yake ya Katibu Mkuu wa CCM hadi anastaafu. Kushoto ni Mke wa katibu huyo, Mama January Makamba.
 Makamu wa Rais wa Jahmuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,akikata utepe kuzindua kitabu cha Binadamu na Kazi, kilichotungwa na Katibu Mkuu Mstaafu wa Chamamcha Mapinduzi CCM, Yusuph Makamba (kulia) wakati ya uzinduzi huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo Mei 27, 2012, sambamba na hafla ya kumpongeza kwa kuitumikia nafasi yake ya Katibu Mkuu wa CCM hadi anastaafu. Kushoto ni Mke wa katibu huyo, Mama January Makamba.
Makamu wa Rais wa Jahmuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,akionyesha Kitabu cha Binadam na kazi baada ya kukizindua kitabu hicho kilichotungwa na Katibu Mkuu Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Yusuph Makamba (kulia) wakati ya uzinduzi huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo Mei 27, 2012, sambamba na hafla ya kumpongeza kwa kuitumikia nafasi yake ya Katibu Mkuu wa CCM hadi anastaafu. Kushoto ni Mke wa katibu huyo, Mama January Makamba.
 Makamu wa Rais wa Jahmuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,akionyesha Kitabu cha Ukweli kwa Mujibu wa Biblia, Kuran Tukufu, Suna za Mtume na Sheria za Nchi,  baada ya kukizindua kitabu hicho kilichotungwa na Katibu Mkuu Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Yusuph Makamba (kulia) wakati ya uzinduzi huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo Mei 27, 2012, sambamba na hafla ya kumpongeza kwa kuitumikia nafasi yake ya Katibu Mkuu wa CCM hadi anastaafu. Kushoto ni Mke wa katibu huyo, Mama January Makamba.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza jambo na Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM, Yusuph Makamba, wakati wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa vitabu vya Ukweli kwa Mujibu wa Biblia, Kuran Tukufu, Suna za Mtume na Sheria za Nchi na Binadam na kazi, vilivyotungwa na Katibu huyo. Uzinduzi huo umefanyika leo Mei 27, kwenye Ukumbi wa Karimjee Dar es Salaam.
Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo.Picha na Muhidin Sufiani-Ofisi ya Makamu wa Rais

Clouds FM Live

Follow by Email

Blog Archive

Popular Posts

MATANGAZO

Followers

How to make a Website